Jumuiya ya Watu wenye Uwalbino Zanzibar (JWUZ)

Jumuiya ya Watu wenye Uwalbino Zanzibar (JWUZ) wameshauriwa kuzijali sana Afya zao na kuzitunza vyema Ngozi zao hususani katika kipindi cha Jua kali ili kujiepusha na Maradhi ya Ngozi na Magonjwa mengine.

Hayo ameyasema Daktari Bingwa wa maradhi ya ngozi Dr Hafidh S. Hassan  katika Clinic ya maradhi ya Ngozi Hospitali ya Mnazi Mmoja wakati akitoa huduma kwa wagonjwa wa matatizo ya ngozi wakiwemo Albino.

Aidha Dr. Hafidh amegawa baadhi ya Vifaaa kwa watu wenye ulemavu wa ngozi kwa ajili ya kujikinga na mwanga mkali wa Jua ikiwemo miwani,kofia  pamoja na lotion ambavyo ni muhim kwao kwani Jua huathiri Ngozi zao na Macho.

Nao Viongozi wa Jumuiya hiyo wamewaomba washiriki wenzao kujitokeza kwa wingi katika Clilic yao kwani wanapata kujifunza mambo mengi yanayohusiana na matatizo ya ngozi hasa kwa watu wenye ulemavu wa ngozi.

 Dr.Hafidhi

Daktari Bingwa wa Maradhi ya Ngozi Dr Hafidh S. Hassan, akitoa maelekezo namna ya kujikinga juu ya maradhi ya Ngozi.

alibino1

Baadhi ya watu waliofika katika Clinic ya Ngozi hospitali ya Mnazi Mmoja  wakitoa shukurani za dhati kwa Uongozi wa Hospitali na Madakitari kwa huduma wanazozipata wanapofika clinic.

Read 572 times

Partners

Social media

f  I

Mnazi Mmoja Hospital map Location

Contact us

Mnazi Mmoja Hospital

Stone Town-Vuga Street

P.O.BOX 672

Tel: +255773833768 / +255627600600

Fax: +255 24 2231613

Email: This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.

Web: www.mmh.go.tz